Monday, August 1, 2016

BAADA YA PROTINI KWENYE MAZIWA YA MENDE, WATAFITI WASEMA MIGUU YAKE PIA NI DAWA.

Baada ya uchunguzi wa kisayansi kubaini kwamba maziwa ya mende yana protini mara nne zaidi ya maziwa ya ng’ombe na kifaru, imebainika kwamba maziwa ya mende pia hutumika kwa matibabu mbalimbali ya binadamu.

Miongoni mwa matibabu hayo ni pamoja na kutengeneza miguu bandia ya kutumiwa na binadamu, mtafiti mkuu katika mradi uliofanyika katika Chuo Kikuu cha A&M cha Texas Hong Liangnchini Marekani amesema…….>>> ‘Nilipoona hii kwa mara ya kwanza nilishangaa’

Alisema wanasayansi kwa miaka mingi wamekua wakishangazwa na uwezo wa mende wa kukaa muda mrefu maeneo yenye sumu na uchafu bila kudhurika, wamegundua kwamba huwa wanatoa kemikali za kupambana na sumu.

Wanaweza kusaidia katika kutengeneza dawa za kusaidia binadamu kukabiliana na bakteria wanaoathiri zaidi watu kwa mfano E.Coli na MRSA ambao hawauliwi kwa dawa yoyote.

Hii siyo mara ya kwanza mende kuhusika kwenye matibabu, Mwandishi Lafcdio Hearn Karne ya 19, alipitia maeneo ya kusini mwa Marekani na kuripoti jinsi watu wenye pepopunda walivyokua wakipewa chai iliyotengenezwa kwa kuwekwa kwa mende aliandia kuwa …….>>>’Sijui ni mende wangapi hutumiwa hadi upate kikombe cha chai, lakini wakazi wa New Orleans wana imani na tiba hiyo’

Pia alisema China kuna mafuta yanayotengenezwa kwa kutumia ungaunga wa mende. Hutumiwa kutumiwa vidonda vya moto pia humezwa kutibu vidonda tumbo. Kuna aina 4500 ya mende na aina nne pekee ambao huwa waaribifu.

Sunday, July 31, 2016

UFAHAMU UGONJWA HUU,WATU WENGI WANAUMWA NA HAWAJIJUI.

Anaandika Dr.Chriss Cyrilo (Daktari wa binadamu).
_____________________________________________

UFAHAMU UGONJWA WA "NARCISSISTIC PERSONALITY DISORDER".

By Dr.Christopher Cyrilo (MD)

Umewahi kusikia ugonjwa wa akili uitwao 'Narcissistic personality disorder (NPD).?' Huenda hujawahi kusikia jina hilo lakini pengine umewahi kuona mtu mwenye dalili za ugonjwa huo. Kadri utakavyoendelea kusoma utaweza kuoanisha dalili za ugonjwa huu na jamii unayoishi nayo na kuona kati ya jamaa zako kama kuna yeyote anayeugua gonjwa hili hatari la akili.

Ugonjwa huu huwaathiri sana watu wazima na hususani viongozi wa taasisi mbalimbali lakini zaidi taasisi za kisiasa. Wapo baadhi ya viongozi wa taasisi nyingine kama vile za dini, elimu, mashirika, makampuni ambao huweza kuugua pia lakini wahanga wakubwa wa ugonjwa huu ni viongozi wa kisiasa.

DALILI ZAKE:
1. Dalili mojawapo za gonjwa hili ni kuwa mtu wa kujisifu na kujivuna (self centered and egoistic), kupaniki, kudharau wengine na kupuuza hisia zao.

2. Mgonjwa huhisi kuwa yeye tu ndio mtu muhimu kuliko wengine na mawazo yake ni sahihi kuliko mawazo ya wengine, na hakuna mjadala. 

3. Maneno na vitendo vya wagonjwa wa Narcissistic Disorder hulenga tu kwenye kujijengea umaarufu na mafanikio binafsi na kutaka kupendwa na watu.

4. Wagonjwa hawa wanapokuwa viongozi, hutumia zaidi vyombo/watu wanaomuunga mkono kukandamiza watu wasiomuunga mkono.

5. Wagonjwa wa aina hii huchagua maneno ya vitisho na mbinu za kuogofya ili kujipa nafasi ya kutamba katika ulingo wa siasa bila changamoto kutoka kwa wapinzani wake.
Mifano ya viongozi wa aina hii ni Idd Amin Dada wa Uganda na  Adolf Hitler wa Germany. Na hao pia walikuwa na wafuasi wengi pamoja na matendo yao yasio ya kawaida.

ATHARI ZAKE:
Wataalamu wa saikolojia wanashauri kuwa, wagonjwa wa "Narcissistic personality disorder" hawapaswi kuwa viongozi wakubwa wa kisiasa. Wanafaa kuongoza familia, kampuni, vikao vya ukoo au jumuiya ndogondogo ambapo watu ni wachache na mawazo kinzani ni nadra.

Lakini wanapopewa majukumu ya kuongoza mataifa/nchi au taasisi kubwa ambapo watu ni wengi na kuna mawazo mengi kinzani huweza kuleta maafa makubwa sana ikiwemo umwagaji wa damu.

Mbaya zaidi, watu wenye gonjwa hili huweza kujiona watakatifu, wapenda watu na watu wazuri, tofauti na matendo yao.

MATIBABU:
Matibabu ya ugonjwa huu ni magumu sana kwa sababu mgonjwa huwa hajui kama anaumwa, na hata ukiambiwa huwa hakubali. Wengi wanaougua ugonjwa huu ukiwaambia wao ni wagonjwa wanaweza kukuadhibu.

Wagonjwa wa aina hii hupatiwa matibabu maalumu ya mazoezi ya akili (psychotherapy) kutoka ka wataalamu waliobobea (Psychotherapist). Hakuna dawa mahususi ya kumeza kwa wagonjwa wa aina hii, lakini kama hali itakua mbaya wanaweza kutibiwa kwa kutumia #antidepressants au #antianxiety.

SWALI;
Je, katika jamii yako unayoishi umewahi kuona dalili za kuongozwa na mtu mwenye ugonjwa huu wa akili? Je umechukua hatua gani??

Dr.Chriss

TAZAMA KIBONZO HIKI CHA SERIKALI IKIHAMIA DODOMA.

SERIKALI IKIHAMIA DODOMA.

Saturday, July 30, 2016

KWA WANAUME SOMA HII YA HUYU MTAFITI, UTAJIFUNZA KITU.

_*Na, Mtafiti.*_
     _Mwanaume_
           24/07/2016.

MWANAUME  _unatakiwa kujitambua na kujiheshimu  bila kusahau kuutunza ujana wako kwa maneno  yenye hekima na busara ,kama wewe ni kijana na haujaoa na una miaka  25 kwenda juu basi jua wewe ni baba pasipo mtoto jiandae  kuwa baba bora na mume bora kwa matendo na mawazo bila kusahau kuitunza haiba yako ya kiume kwa mavazi safi na bora._

MWANAUME _anayejiheshimu huwa hanyoi kiduku hata siku moja ,kijana bora mwenye kujitambua huwa sio mtumwa wa pombe hata siku moja,kuwa na idadi kubwa ya wanawake sio ujanja bali ni utumwa wa fikra  sababu unatakiwa uitawale pombe na wanawake .sasa ni wakati sahihi wa kuacha ujinga a kujiaanda kuwa mume bora na baba bora._

MWANAUME_ _anayejitambua havai nguo za kumbana mapaja ,havai mlegezo wala   havai nguo za kumbana makalio, mtoto wa kiume  ,jaribu kuwa Muungwana sababu  neno mwanaume limebeba ubora wa utashi wa fikra na tabia ._

_Wanawake wanapenda wanaume wenye upeo mkubwa na  wanao jiamini sababu mwanaume  ni kiogozi na kichwa katika familia sasa unawezaje kuwa kichwa cha familia na kiduku  huku ukiwa na mlegezo ?_

_Wewe ambaye upo  chuo ujanja si kupiga selfie na wanawake   au kushinda kwenye Instagram part kila weekend ,badilika sasa na acha ujinga tumia chuo kama kiwanda cha maarifa na  sio sehemu ya fashion show na mashindano ya kununua smart phone ,kuwa mwanaume bora ili ukikutana na wanaume  wenzio uzungumze kama mwanachuo aliyekomaa nasio kulamba lamba midomo_

_Ongeza idadi ya kusoma vitabu na sio kuwa  mashindano ya kuwa  na idadi  nyingi ya likes za picture za swagger na wingi wa majina yasio na tija ,kumbuka Kendrick Lamar  alitengeneza Brand ya jina lake na wewe tengeneza Brand name yako na sio kuiga ujinga usio na tija.You cannot change yesterday, but you can change today and tomorrow. #Modern Gentleman._

_By Mtafiti._.

Friday, July 29, 2016

18+KWA WANAUME WENYE TATIZO LA KUFIKA HARAKA WAKATI WA TENDO LA NDOA ,TUMIA MBINU HIZI ZITAKUSAIDIA.ACHANA NA MADAWA

Watu wengi wana tatizo hili usiwaone wamevaa masuruali hawasemi tu, kwa machache tu kwa ufahamu mchache nilio nao,Kwanza fanya mazoez ya kuzuia kukojoa...mimi binafsi niliwah kupiga nyeto kwa vipindi tofaut huko nyuma......ila nilikua napenda sana ile raha ya kutaka kumwaga niendelee kuisikia japo kwa dakika kadhaa,.........kumbe kule kujichelewesha kulinipa ex[perience nyingine!!nilijikuta baada ya muda fulani ninauwezo wa kukontroo nikojoe baada ya muda gani,,,nilipoingia rasmi kwenye uhusiano na laazizi wangu aliniona pamoj ana sifa nyingine zakipekee nilizo nazo kuwa mwanaume wake never seen....si kwamba najisifia ndugu ila nina uwezo kwa kukaa juuya kifua cha mwanamke hata kwa dakika 30...bila kupiz na hapo ni hadi aniambie plz beby come..try that na uniambie..pili jua Mwili ukiwa kwenye hali nzuri kiafya na tendo huwa linaenda ipasavyo. Na mwili ukiwa dhoofu basi tegemea tukio dhoofu pia. Hivyo ukitaka kuwa na matokeo mazuri kwenye ndoa yako, jitahidi sana kujiweka vizuri kwa kula sahihi na kufanya mazoezi mepesi mepesi tu kwa wale wanaoweza kuutumia muda vizuri wapiti pite Gym walau siku mbili na kuendelea kwa wiki. Kufahamu kuwa kupumzika kwa uume baada ya baada kufika mara ya kwanza sio tatizo. Kwa wanaume walio wengi, baada ya mshindo wa kwanza hupumzika kidogo kabla ya kuendelea na awamu nyingine. Japo kuna ambao wana uwezo wa kuendelea moja kwa moja bila kupumzika (law ya use and misuse inahusika kwa wengine apa). Kwa hio kusinyaa kwa uume baada ya mshindo wa kwanza, isifahamike kuwa ni upungufu wa nguvu bali ni ajdustiment ya mwili wenyewe kutokana na kwamba mwanaume kabla ya tendo mapigo ya moyo huongezeka na huchangia damu kwenda kwa kasi, na kwa hali hio anakua yupo juu sana kimhemko, inapofikia anamaliza raundi ya kwanza mwili unakua unapoa /umesharudi kwenye hali yake ya kawaida, ndiko kunakosababisha hio maneno kusinyaa kwa wengi wakati mapigo ya moyo yanaporudi kawaida (MWILI KUPOA). Maandalizi ya mwili. Wanaume tupo tayari muda wote… ila linapokua swala ya mwenza wako (kwa kuwa muda unaotumia kwa maandalizi na tendo una uhusiano wa moja kwa moja na satisfaction ya mwenzio)… unahitaji muda angalao nusu saa na kuzidi kujiandaa na mwenzi wako. Kama timu ya mpira inapoenda ugenini huhitaji muda kuzoea mazingira, ndio na mwanaume anavyohitaji muda kuzoea mazingira ya ugenini. Hili linakusaidia sana mwanaume kutoka kwenye mihemko na kurudi kwenye hali yako ya kawaida ambayo itakusaidia kuwa na muda mzuri zaidi wa kufurahia tendo. Jitahidi pia kuvuta pumzi nyingi ndani na uiachie polepole kukusaidia kukuweka kwenye utulivu mzuri. Timing ya kuanza tendo: Kwa kuwa tendo linahusisha sana hisia za mwili, ukiwa umetumia muda unaotosha kuandaana, basi usiwe na papara mwanzoni, bali uwe na utulivu, pia jitahidi kuzungumza moja mawili wakati unaanza kuzoea mazingira mengine (core business) EPUKA UHARAKA na kuweka sana akili yako hapo, jinafikie mwenyewe kuwa its just a normal thing (mental pride) Concetration/ Umakini uliopitiliza… Unapaswa kumfanya mkeo aweke akili yake yote hapo, na wewe unatakiwa katika kumuweka mkeo kwenye concentration uuharibu umakini wako (level of concentration). Ukiweka concentration ya juu sana kwenye tendo… haikuchukui dakika mbili umemaliza, na kuirudisha tena ile hali ya concentration uliokua nayo mwanzo itakuwia ngumu sana….. Usiweke sana akili yako hapo kama unataka kufurahia kwa muda zaidi. ila kama hutaki kudumu.. weka akili na umahini wako hapo woote.. just seconds or a minute you are done MAZOEZI ya mwili ni muhimu sana sana sana sana sana kwetu wanaume. Kama huna muda wa kwenda jimu walau ukiamka piga ‘PUSH-UPS walau 50’’ kila siku na ‘’SQUARTS’’ . haya ni mazoezi mepesi lakini ni BORA zaidi kwa mwanaume. Kwetu sisi wanaume tunatumia sana misuli yetu wakati huu, kwa hio kuna ulazima wa kutafuta ustahimilivu wa misuli ''mussle strength n perseverance''. Hio kitu ni starehe na unatakiwa baada ya tendo uwe umekuwa refreshed na sio uwe unaumwa kila mahali na sijui joints zinauma sijui nini nini? ukijiona unakuwa hivyo baada ya tendo ujue mwili wako haujakaa fiti ipasavyo kimazoezi/kiafya Pia Afya ya Akili inahusika sana, Japo inahitaji jitihada makhususi... lakini kila mtu ana uwezo wa kuchagua nini cha kufikiria na nini si cha fikiria(kupuuzia) na pia akienda hatua zaidi anaweza kupuuza kila kitu kwa wakati fulani kama unajua una huo uwezo na ukaamua kuutumia. Pia kuchagua kufikiri yale yaliopo kwenye uwezo na urefu wa kamba yako pekee; vitu usivyo na uwezo navyo utajisumbua tu bure na kujipa stress zaidi. Weka nguvu na jitihada zako kwenye kutafuta ufumbuzi wa changamoto zako, jifunze na acha kufikiria matatizo kwa maana hakubadilishi kitu na yataendelea kuwa hivyo n.k n.k................ Ukiwa na namna nzuri ya kuyachanganua mambo yako utasaidika sana kwenye afya ya akili yako na kuwa vizuri zaidi

Thursday, July 28, 2016

UTAFITI: Kutazama TV kunaweza kusababisha kifo.

Utafiti huu umeripotiwa na BBC ambapo imeelezwa kuwa umefanywa na wanasayansi wa Japan ambapo umethibitisha kwamba kukaa kwa muda mrefu na kutazama vipindi vya televisheni kwa saa nyingi  kunahatarisha afya kwani kunahusishwa na maradhi yanayosababisha mzunguko wa damu mwilini kutokuwa sawa.

Watafiti hao wamesema hali hiyo pia huenda ikasababisha damu kuganda na kutengeneza vidonge katika sehemu kama vile miguu, na iwapo mgando huo utasukumwa na nguvu za mzunguko wa damu na kuingia sehemu kama vile mapafu husababisha vifo.

Utafiti huo ulihusiha watu zaidi ya 86,000 ambao hupendelea kutazama televisheni katika mida mbalimbali kwa siku. Kisha afya zao zilifuatiliwa kwa zaidi ya miezi 19 tangu mwaka 1988 hadi 1990.

Matokeo yalikuwa kila muda wa masaa mawili yalipopita mtu akikaa kutazama televisheni, hatari ya kupata ugonjwa wa mapafu uitwao ‘Fatal pulmonary embolism’ ulioongezeka kwa asilimia 40.

Iligundulika pia kuwa waliotazama vipindi vya televisheni kwa zaidi ya saa 5 walikuwa katika hatari zaidi kuliko waliotazama televisheni kwa muda wa chini ya saa 3.

Aidha watu huambatanisha kitendo cha kukaa na kutazama televisheni huku wakila vitafunio kama vile Popcorns na Crisps ambavyo pia huwasababishia si tu mwili kukosa mazoezi bali pia kuongezeka kwa uzito unaohatarisha afya.

JE WAJUA WATANZANIA WENGI HUTAFUTA NINI KWENYE MTANDAO??

Maendeleo ya sayansi na Teknolojia yameleta neema na mapinduzi makubwa Duniani. Tofauti na nchi zilizoendelea ambazo zimeingia kwenye ulimwengu wa mtandao muda murefu, Suala la mtandao linaonekana Jipya kwa watanzania walio wengi, na Wengi wao wanataman kuona kuna nini huko ndani? Ujio wa simu za kisasa (smartphones) umekuwa jibu na suluhisho la tatizo hilo.

JE WAJUA WATANZANIA HUTAFUTA NINI KWENYE MTANDAO?

Hivi ni Vitu Kumi Zaidi Wanavyovitafuta Watanzania (Kwa mujibu wa Kitafutio cha Google)

10.Biashara
Kutokana na kukua kwa kasi kwa uuzaji na ununuzi pepe (e-commerce) duniani, watanzania hawajaachwa nyuma sana japo ni idadi ndogo sana ya watanzania wanaoweza kufanya biashara mtandaoni. Wengi wa watanzania hutafuta na kuuza Magari, Simu za mkononi, pikipiki, nyumba na maeneo ya ardhi.

9.Vichekesho (comedy)
Utashangaa lakini hii ni moja ya vitu ya vitu vinavyotafutwa sana na Watanzania wengi kwenye mtandao, Wengi hutafuta video za kuchekesha, picha, na meseji za vichekesho. pia hupenda kuwajua wachekeshaji nk.

8.Elimu, mafunzo na afya
Kwa kiasi fulani kuna idadi ya watu wanaoingia kwenye mtandao kupata elimu inaongezeka, japo wahusika wengi hapa huwa wanafunzi hasa wa vyuoni ambao wengi hutumia google kupata majibu ya maswali waliyopewa na wakufunzi wao!

7.Michezo
Utakubaliana na mimi  kwamba watanzania wengi ni wapenda michezo (JAPO HAWAPENDI MAZOEZI YA VIUNGO) Wengi wa Watanzania huingia mtandaoni kupata habari za soka hasa za bara la ulaya.

6.Siasa
Uelewa wa Watanzania katika Siasa umekua ukiongezeka siku hadi siku na kumekuwa na idadi kubwa sana ya Watanzania wanaotafuta habari za siasa mfano; bunge, bajeti ya nchi, mahusiano ya nchi yetu na mataifa mengine, Vyama vya siasa nk.

5. Mahusiano & Kutafuta wapenzi
Kama ilivyo kwa nchi nyingi Duniani, Kumekuwa na idadi kubwa sana ya watu wanaotembelea mitandao ya kutafuta wapenzi, ushauri wa mapenzi, nk japo kuna unafuu kwetu (pengine ni kutokana na kutokuwa na uwezo wa kupata intaneti) kulingananisha ni nchi zingine kama nigeria na kenya.

4. Kutafuta Video, Muziki , na Programu za computer/simu
Kuna idadi kubwa sana ya Watanzania Wanaotafuta vitu hivi, Cha ajabu na Kwamba Video nyingi zinazotafutwa ni zile zenye maudhui ya kikubwa (adult movies). Pia nyimbo Zinazoangaliwa zaidi youtube ni zile zinazoonesha watu wakicheza bila maadili.

3. Kusoma na Kutuma Barua pepe
Watanzania walio na uwezo wa kuingia mtandaoni, Wengi wao wana anuani za Barua pepe japo ukweli ni kwamba kati ya watanzania 10 wenye anuani za barua pepe, ni watanzania watatu (3) tu ndio wenye Uelewa juu ya barua pepe na kuzitumia. 7 waliobaki pengine walifungua anuani ya barua pepe kwa kushurutishwa au ili tu wajiunge na mtandao fulan wa kijamii hasa facebook.

2.Blog na Magazeti
Blog na Magazeti zinashika nafasi ya pili kati ya vitu vinavyosomwa zaidi na watanzania kwenye Mtandao. Watanzania wengi hupenda kujua habari muhimu kuhusu yanayoendelea nyumbani na kimataifa pia, michezo, burudan nk. Watanzania pia hupenda kuangalia watu fulani mashuhuri kupitia blogs mbalimbali.

1. Mitandao ya kijamii
Najua utakubaliana na mimi kwamba karibu kila mwenye uwezo wa kuingia mtandaoni basi ameshajiunga na moja kati ya mitandao ya kijamii kama facebook, twitter, LinkedIn, Instagram, nk. Hii ndio inayoongoza kutembelewa na watanzania walio wengi zaidi kuliko kingine chochote.

THE 8 MONKEYS .

The 8 Monkeys (This is reportedly based on an actual experiment conducted.) Put eight monkeys in a room. In the middle of the room is a ...